Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

Rouhani atuma salamu za rambirambi kwa Wanepal

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Nepal kutokana na maafa yaliyosababishwa na mtetemeko wa ardhi uliotokea jana nchini humo na kuua karibu watu elfu mbili.
Ujumbe wa Rais Rouhani kwa mwenzake wa Nepal, Ram Baran Yadav umesema Iran imesikitishwa na kuhuzunishwa sana na habari ya tetemeko la ardhi na vifo vya idadi kubwa ya watu wa Nepal. Rais Rouhani ameongeza kuwa, sambamba na kutoa salamu za rambirambi kwa rais, taifa la Nepal pamoja na ndugu wa wahanga wa tetemeko hilo, anawatakia ahueni waliojeruhiwa na kuwaombea dua njema.
Ripoti za hivi karibuni zinasema kuwa mtetemeko mkubwa wa ardhi uliotokea jana karibu na mji mkuu wa Nepal, Kathmandu umeua watu wasiopungua 1900.
Wakati huo huo Jumuiya ya Hilali Nyekundu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa iko tayari kutuma misaada ya dharura kwa watu walioathiriwa na mtetemeko wa jana nchini Nepal

No comments:

Post a Comment