Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 21 April 2015

13 wauawa katika mashambulio ya Saudia Yemen

Watu 13 wamepoteza maisha yao nchini Yemen kufuatia mashambulio ya anga ya vikosi vamizi vya Saudi Arabia. Mashambulio hayo ambayo yamepelekea pia watu wasiopungua 70 kujeruhiwa yalilenga maeneo ya soko na makazi ya raia katika mji wa Haraz, kaskazini magharibi mwa jimbo la Hajjah. Msemaji wa Harakati ya wananchi ya Ansarullah amesema kuwa, mashambulio ya utawala wa kifamilia wa Aal Saud dhidi ya wananchi wa Yemen ni jinai dhidi ya binadamu. Muhammad Abdus Salaam amebainisha kwamba, hatua ya Saudia ya kuwauwa kwa umati wananchi wa Yemen na kutokomeza miundo mbinu muhimu ya nchi hiyo umeufanya utende jinai mbaya kabisa dhidi ya binadamu. Wakati huo huo vyama vinavyounda Muungano wa Kitaifa wa Demokrasia nchini Yemen vimetangaza kuwa, Saudi Arabia imepuuza matakwa yote ya kimataifa ya kusitisha mauaji dhidi ya raia wa Yemen na kuacha kuharibu miundo mbinu ya nchi hiyo. Vyama hivyo aidha vimelaani mashambulio hayo ya Saudia ambayo yamekuwa yakiwauwa raia wasio na hatia yoyote na kusisitiza kwamba, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linapaswa kuichukulia hatua Saudia kutokana na kutenda jinai dhidi ya binadamu

No comments:

Post a Comment