Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 26 April 2015

Wabenin wapiga kura kuwachagua wabunge

Mamilioni ya wananchi wa Benin leo wameeleka kwenye masanduku ya kupigia kura kuwachagua wawakilishi wao katika bunge la nchi hiyo.
Kamisheni ya Uchaguzi ya Benin imetangaza kuwa Wabenin karibu milioni 4 wametimiza masharti ya kupiga kura na kwamba wabunge 83 watachaguliwa moja kwa moja katika uchaguzi wa leo.
Umoja wa Afrika (AU) umetuma maafisa 40 kwa ajili ya kusimamia zoezi hilo la uchaguzi, kuhesabiwa kura na utangazaji wa matokeo yake. Ujumbe huo unaongozwa na rais wa zamani wa Mali.
Uchaguzi wa Bunge nchini Benin unafanyika siku chache tu baada ya chaguzi za rais zilizofanyika kwa amani na utulivu katika nchi za Togo na Nigeria, jambo ambalo limetajwa kuwa ni ishara ya kuimarika demokrasia barani Afrika

No comments:

Post a Comment