Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 25 April 2015

Tetemeko kubwa la ardhi laua watu 1,400 nchini Nepal

Zaidi ya watu 1,400 wamepoteza maisha yao kufuatia mtetemeko mkubwa wa ardhi wenye ukubwa wa 7.9 kwa kipimo cha rishta uliotokea magharibi mwa Nepal karibu na mji mkuu Kathmandu. Mtetemeko huo uliotokea majira ya mchana kwa wakati wa Nepal umeutikisa vibaya mji mkuu Kathmandu ambapo mbali na kupelekea mamia ya watu kupoteza maisha na maelfu ya wengine kujeruhiwa, umesababisha uharibifu mkubwa wa nyumba. Waziri wa Habari wa Nepal Minendra Rijal amewaambia waandishi wa habari kwamba, mji mkuu Kathmandu ndio ulioathiriwa zaidi na baa hilo la kimaumbile. Idadi ya waliopteza maisha katika mtetemeko huo wa ardhi inakadiriwa kuwa, itaongezeka hasa kutokana na kuwa, watu wengi wamefukiwa na vifusi. Habari zaidi zinasema kuwa, majengo na majumba mengi yakiwemo ya kihistoria yamebomolewa na kuharibiwa kabisa na tetemeko hilo la ardhi. Waziri wa Habari wa Nepal amesema kuwa, timu maalumu ya uokozi tayari imetumwa katika maeneo yaliyokumbwa na mtetemeko huo wa ardhi na kwamba, kazi ya uokozi inaendelea. Mtetemeko huo wa ardhi umeitikisa pia nchi jirani ya Bangladesh na taarifa kutoka nchini humo zinasema, watu wawili wamepoteza maisha na wengine mia moja wamejeruhiwa kufuatia janga hilo la kimaumbile. Aidha mji mkuu wa India New Delhi na baadhi ya miji ya mashariki mwa nchi hiyo nayo imekumbwa na mtetemeko huo wa ardhi.

No comments:

Post a Comment