Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 15 May 2015

Jeb Bush aambiwa: 'Kaka yako aliunda ISIS'

Jeb Bush Jeb Bush
Mwanafunzi wa chuo kikuu nchini Marekani amemlaumu vikali mgombea tarajiwa wa kiti cha urais kwa tiketi ya chama cha Republican Jeb Bush na kumfahamisha bayana kuwa kundi la kigaidi la ISIS (Daesh) liliundwa na kaka yake, rais wa zamani wa Marekani George W. Bush.
Tukio hilo limejiri katika mkutano wa kampeni katika jimbo la Nevada siku ya Jumamosi baada ya Jeb Bush kumaliza mkutano huo. Jeb Bush aliwahi kuwa Gavana wa Florida na anatazamiwa kutangaza azma yake ya kuwania urais katika uchaguzi ujao wa rais mwaka 2016.
Ivy Ziedrich, mwanaharakati wa kisiasa, alimbana vikali Jeb kuhusu hatua ya George W Bush kuvamia Iraq na hatimaye kuunda kundi la kigaidi la ISIS. Mwanaharakati huyo amemfahamisha Jeb Bush kuwa kaka yake alivamia Iraq na kuwaachia kwa makusudi wanamgambo wapate silaha za kisasa.
Jeb Bush alipinga kauli hiyo, hata hivyo alisema kuna baadhi ya makosa yaliyofanywa na rais wa wakati huo wa Marekani katika kutuma majeshi nchini Iraq.

No comments:

Post a Comment