Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 12 May 2015

Wanajeshi wanane wa Mali wauawa Timbuktu

Wanajeshi wasiopungua wanane wa Mali wameuawa na wengine 10 kujeruhiwa katika shambulio lililofanywa na waasi wa nchi hiyo karibu na mji wa Timbuktu wa kaskazini mwa nchi hiyo.
Duru za kuaminika zimeripoti habari hiyo na kusema kuwa shambulio hilo lilifanywa jana na waasi wa Tuareg.
Afisa mmoja wa masuala ya misaada ya kibinadamu katika eneo hilo amesema kuwa, waasi wanaopigania kujitenga eneo la Azawad kwa kifupi CMA walipambana na wanajeshi wa serikali jana asubuhi ambapo wanajeshi wanane waliuawa na wengine 10 kujeruhiwa.
Kwa mujibu wa afisa huyo, magari mawili ya jeshi la Mali yamechomwa moto na waasi hao.
Jeshi la Mali limekataa kutoa maelezo rasmi kuhusu habari hiyo ingawa hata hivyo afisa mmoja wa kikosi cha dhiba cha jeshi la Mali kilichotumwa katika eneo hilo amethibitisha habari hiyo.

No comments:

Post a Comment