Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 19 December 2014

Marekani ilitaka kushambulia vinu vya nyuklia China

Nyaraka za siri zilizokuwa zimefichwa kwenye masjala ya Wakala wa Usalama wa Taifa wa Marekani NSA zinaonyesha kuwa, Marekani ilikuwa na mpango wa kushambulia kwa makombora vinu na mitambo ya nyuklia ya China. Taarifa zinasema kuwa, Marekani ilichukua uamuzi wa kuvishambulia kwa makombora vinu na mitambo ya nyuklia ya China wakati wa tawala za marais John F Kennedy na Lyndon B. Johnson katika muongo wa sitini. Nyaraka hizo za siri zinaonyesha kuwa, aliyekuwa Mkuu wa Kamisheni ya Nyuklia ya Marekani kuanzia mwaka 1961 hadi 1971 alithibitisha juu ya kutaka kufanyika shambulio hilo dhidi ya mitambo ya nyuklia ya China. Mkuu huyo alieleza kwenye nyaraka hizo kwamba uamuzi huo wa Marekani ulichukuliwa baada ya China kukataa kujiunga kwenye makubaliano ya upigaji marufuku majaribio ya silaha za nyuklia. Taarifa hizo zinaeleza kuwa, Umoja wa Kisovieti wa Urusi ya zamani pia ulikubali kushirikiana na Marekani kwa ajili ya kuvishambulia vinu vya nyuklia vya China. Hata hivyo, Marekani ilishindwa kutekeleza azma yake hiyo kwa hofu kwamba China ingelitoa radiamali kali dhidi ya Taiwan, inayohesabiwa kuwa mshirika mkubwa wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Mbali.

No comments:

Post a Comment