Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 15 May 2015

Mauaji ya kutatanisha mashariki mwa DRC

Habari kutoka mji wa Beni, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zinasema kuwa watu wasiopungua 20 wameuawa katika mazingira ya kutatanisha katika kipindi cha siku tatu zilizopita. Mashuhuda wameiambia idhaa hii kwamba maiti za watu 20 zilizokatwa vipande vipande zimetapakaa katika vichaka na misitu ya karibu na mji wa Beni na kwamba serikali imesisitiza kuwa waasi wa kutoka Uganda wa ADF-Nalu ndio waliotekeleza mauaji hayo. Hii ni katika hali ambayo, jeshi la DRC miezi miwili iliyopita lilitangaza kuwa limeharibu ngome nyingi za waasi hao katika maeneo mengi hususan katika mikoa ya Kivu Kusini na Kaskazini inayopatikana mashariki mwa nchi hiyo.
Eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limekuwa likikumbwa na mauaji yanayotokana na hujuma za makundi ya waasi; na wafuatiliaji wengi wa mgogoro wa nchi hiyo wanasema waasi hupiga kambi mashariki mwa DRC kutokana na eneo hilo kuwa na rasilimali nyingi kama vile madini yenye thaman

No comments:

Post a Comment