Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 11 May 2015

Afkham: Madai ya Ahmad Shaheed ni urongo mtupu

Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, madai ya Ahmad Shaheed, Ripota Maalumu wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Masuala ya Iran kwamba, hapa nchini kumekuwa kukitekelezwa unyongaji wa watu kwa siri na kunyongwa pia wafungwa wa kisiasa ni urongo mtupu. Marzieh Afkham amebainisha kwamba, madai hayo yanakinzana wazi na majukumu yake. Afkham amesema, Iran imebainisha mara chungu nzima kwamba, Ahmad Shaheed amekuwa akitegemea vyanzo vya uongo katika kuandaa ripoti zake ambazo zinapingana na uhalisia wa mambo. Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amebainisha kwamba, inasikitisha mno kwamba, utendaji kazi wa Ripota Maalumu wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Masuala ya Iran hauko katika mkondo sahihi na hautegemei ushahidi wa kweli. Amesema, madai hayo ya mara kwa mara dhidi ya Iran yana malengo ya kisiasa.

No comments:

Post a Comment