Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema
kuwa: Uandikaji wa matini ya makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na
kundi la 5+1 unaendelea vizuri, ijapokuwa bado kuna masuala mengi
yaliyosalia. Muhammad Jawad Zarif amesema kuwa, mazungumzo ni magumu,
lakini amesisitiza kwamba Iran na kundi la 5+1 zina nia ya kweli ya
kutatua migogoro migumu ili kufungua kurasa mpya. Pande hizo mbili za
mazungumzo ya nyuklia zilianza kazi ya kuandika matini ya makubaliano ya
nyuklia Alkhamisi iliyopita huko New York Marekani.
Mazungumzo hayo yanafanyika kwa kuhudhuriwa na Sayyid Abbas Araqchi na Majid Takhte Ravanchi, Manaibu Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Helga Schmid, Naibu Mtaribu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya. Sayyid Abbas Araqchi, afisa mwandamizi katika timu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran pia amesema kuwa anataraji kwamba rasimu ya makubaliano kamili itakuwa tayari, ingawa kutakuwepo na masuala mengi yaliyosalia kwenye rasimu hiyo.
Mazungumzo hayo yanafanyika kwa kuhudhuriwa na Sayyid Abbas Araqchi na Majid Takhte Ravanchi, Manaibu Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Helga Schmid, Naibu Mtaribu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya. Sayyid Abbas Araqchi, afisa mwandamizi katika timu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran pia amesema kuwa anataraji kwamba rasimu ya makubaliano kamili itakuwa tayari, ingawa kutakuwepo na masuala mengi yaliyosalia kwenye rasimu hiyo.
No comments:
Post a Comment