Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 4 May 2015

Uandikaji matini ya makubaliano waendelea vyema

Zarif Zarif
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa: Uandikaji wa matini ya makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1 unaendelea vizuri, ijapokuwa bado kuna masuala mengi yaliyosalia. Muhammad Jawad Zarif amesema kuwa, mazungumzo ni magumu, lakini amesisitiza kwamba Iran na kundi la 5+1 zina nia ya kweli ya kutatua migogoro migumu ili kufungua kurasa mpya. Pande hizo mbili za mazungumzo ya nyuklia zilianza kazi ya kuandika matini ya makubaliano ya nyuklia Alkhamisi iliyopita huko New York Marekani.
Mazungumzo hayo yanafanyika kwa kuhudhuriwa na Sayyid Abbas Araqchi na Majid Takhte Ravanchi, Manaibu Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Helga Schmid, Naibu Mtaribu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya. Sayyid Abbas Araqchi, afisa mwandamizi katika timu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran pia amesema kuwa anataraji kwamba rasimu ya makubaliano kamili itakuwa tayari, ingawa kutakuwepo na masuala mengi yaliyosalia kwenye rasimu hiyo.

No comments:

Post a Comment