Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 24 May 2015

Vikosi vya Iraq vyasonga mbele kuelekea al Ramadi

Vikosi vya jeshi la Iraq vikishirikiana na vikosi vya kujitolea vya wananchi vinasonga mbele kuelekea mji wa Al Ramadi, wiki moja baada ya mji huo kushikiliwa na wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh. Afisa mmoja wa Polisi na mpiganaji wa makabila ya Kisuni wamesema, kwa msaada wa wanamgambo wa Kishia, vikosi vyao vimeukomboa mji wa Husaiba al-Sharqiya ulioko umbali wa kilomita 10 mashariki mwa Al Ramadi kutoka mikononi mwa magadi wa Daesh. Amir al-Fahdawi, kamanda wa vikosi vya makabila ya Iraq amesema, leo wameukomboa mji wa Husaiba al-Sharqiya, huku wakiandaa mikakati ya kuwarejesha nyuma zaidi wapiganaji wa kundi la kigaidi la Daesh. Kwa mujibu wa kamanda huyo, ndege za kivita za jeshi la Iraq zinaendelea kuzishambulia kwa makombora ngome za kundi la kigaidi la Daesh zilizoko kwenye ufukwe wa Mto Euphrates. Kushikiliwa mji wa Al Ramadi na kundi la kigaidi la Daesh kumetilia shaka athari za mashambulio ya anga dhidi ya ngome za kundi hilo yanayofanywa na muungano wa madola ya kigeni yanayoongozwa na Marekani. Wakati huo huo Muwaffaq al Rabei, mjumbe wa Kamisheni ya Usalama na Ulinzi katika bunge la Iraq amesisitiza kuwa mapambano dhidi ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh yataendelea. Al Rabei amesema mji mkuu wa Iraq, Baghdad uko salama na kwamba kundi la kigaidi la Daesh halina uwezo wa kutia mguu katika mji huo

No comments:

Post a Comment