Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 11 May 2015

UNICEF: Hali ya kibinadamu Yemen ni mbaya

Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetahadharisha kuhusiana na hali mbaya ya kibinadamu inayoikabili Yemen kutokana na uvamizi na mashambulio ya kijeshi ya Saudi Arabia katika nchi hiyo na kusisitiza kwamba, hali ya kibianadamu nchini humo ni mbaya mno. Mohamed al-Asadi, msemaji wa Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) nchini Yemen amesema kuwa, hali ya kibinadamu nchini Yemen inazidi kuwa mbaya siku baada ya siku. Amesema, kutokana na mashambulio ya Saudia kusababisha hasara kubwa, hali ya kibinadamu ni mbaya na kwamba, wananchi wa nchi hiyo wanahitajia misaada zaidi. Tume ya kuchunguza hasara zitokanazo na mashambulizi hayo, imetangaza kuwa zaidi ya watu 2,000 wamekwishauawa na maelfu ya wengine kujeruhiwa. Hayo yanajiri katika hali ambayo, wanajeshi wa Yemen pamoja na wapiganaji wa harakati ya wananchi ya Ansarullah wamekaribisha kwa mikono miwili pendekezo la usitishwaji mapigano kwa muda ili kuruhusu misaada ya kibinadamu kuwafikia raia wa kawaida wanaokabiliwa na matatizo. Usitishaji vita huo wa siku tano utaanza kutekelezwa kesho

No comments:

Post a Comment