Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 8 May 2015

AU yasema hali hairuhusu kufanyika uchaguzi Burundi

Umoja wa Afrika (AU) umeonya leo kuwa hali ya Burundi si mwafaka kwa ajili ya kufanyika uchaguzi na kusema kuwa haitoweza kutuma waangalizi wake nchini humo baada ya malalamiko ya machafuko yaliyosababisha vifo, yaliyochochewa na hatua ya Rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza kuamua kugombea urais kwa kipindi kingine cha tatu. Mkuu wa Kamisheni ya AU Bi Nkosazana Dlamini Zuma amesema mazingira yaliyopo si mwafaka kwa ajili ya uchaguzi na kuongeza kama ninavyomnukuu:”Huwezi kwenda kwenye nchi ambayo unakutana na wakimbizi wanaoondoka, kisha useme, ‘tunakwenda kufanya uangalizi wa uchaguzi’”. Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amebainisha kuwa kutokana na mambo yalivyo haoni hata kama uchaguzi utaweza kufanyika katika mazingira hayo. Kuhusiana na uamuzi wa Mahakama ya Katiba ya Burundi wa kumuidhinisha Rais Nkurunziza kugombea urais kwa muhula wa tatu, Bi Nkosazana Dlamini Zuma amesema, ukiondoa mahakama hiyo, tafsiri nyengine zote wanazopatiwa kuhusiana na katiba ya nchi hiyo zinaonyesha kuwa Rais Nkurunziza hafai kugombea kwa kipindi cha tatu. Wakati huohuo watu wasiopungua wanne wameuawa katika wimbi jipya la machafuko yaliyosababishwa na upinzani dhidi ya hatua ya Rais Pierre Nkurunziza ya kugombea urais kwa kipindi kingine cha tatu. Kwa mujibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu maiti tatu zimeonekana leo kwenye barabara za mji mkuu Bujumbura. Mtu mwengine ameuawa kwa guruneti katika mapigano kati ya polisi, waandamanaji na wanamgambo wanaoiunga mkono serikali wajulikanao kama Imbonerakure. Katika tukio jengine lililotokea kwenye wilaya ya Nyakabiga jijini Bujumbura leo, waandamanaji wanaopinga Rais Nkurunziza kugombea tena urais wamemuua kwa kumvisha matairi ya moto shingoni mtu mmoja, wakisema ni mwanachama wa tawi la vijana la chama tawala ambaye aliwahi kuwashambulia wakati walipokuwa wakiandamana…/
Zaidi katika kategoria hii:

No comments:

Post a Comment