Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 11 May 2015

Zarif: Iran kupanua ushirikiano wake na Afrika Kusini

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kustawisha zaidi ushirikiano wake na Afrika Kusini katika nyanja zote hususan uga wa kiuchumi. Dakta Muhammad Javad Zarif amesema hayo katika mazungumzo yake na Bi Maite Nkoana-Mashabane, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Afrika Kusini ambaye yuko safarini hapa nchini na kuongeza kuwa, licha ya kuweko vikwazo, lakini Iran na Afrika Kusini zinaweza kuwa na ushirikiano katika masuala ya mafuta na kadhalika. Kwa upande wake Bi Maite Nkoana-Mashabane, amesema kuimarishwa ushirikiano wa Tehran na Pretoria ni jambo muhimu na kwamba, lengo la safari yake hapa nchini ni katika kuimarisha uhusiano huo. Aidha akizungumza kwenye kikao cha kamisheni ya pamoja ya uchumi ya Iran na Afrika Kusini Bi Nkoana-Mashabane alisema vikwazo ilivyowekewa Iran si vya kimantiki, vya upande mmoja na havina uhalali wa kisheria.

No comments:

Post a Comment