Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 8 May 2015

Magaidi Syria waungana kupambana na kundi la Daesh

Makundi ya kigaidi kusini mwa Syria yameungana na kutekeleza mashambulizi makali dhidi ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh nchini humo. Habari kutoka kwa magaidi hayo, zimeeleza kuwa, kundi la kitakfiri la Jab’hatu Nusra na makundi mengine yanayopigana dhidi ya serikali halali ya Syria, yaliungana siku chache zilizopita na kutekeleza operesheni kali dhidi ya wanachama wa kundi la Daesh katika eneo la al-Qahtwaniyyah, katika viunga vya mji wa al-Qunaitra, kusini mwa Syria na kufanikiwa kudhibiti ngome muhimu ya wanachama wa kundi hilo. Katika mapigano hayo makali, makumi ya matakfiri wa kundi la Jab’hatu Nusra na Daesh, wameangamizwa huku wengine wengi wakijeruhiwa vibaya. Makundi hayo ya kitakfiri yaliyoungana katika operesheni za kuitwaa ngome hiyo muhimu ya kundi la kigaidi la Daesh, ni pamoja na makundi ya kigaidi ya Jayshul-Islami, Jayshul-Yarmuuk, Jayshul-Awwal na Ahrarush-Sham, yote ya Masalafi wa Kiwahabi ambayo yanapambana dhidi ya serikali ya nchi hiyo. Kwengineko jeshi la Syria kwa kushirikiana na wanamapambano wa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah, limefanikiwa kudhibiti kikamilifu maeneo ya Isal al-Ward lenye upana wa kilometa mraba 45 katika mipaka ya pamoja kati ya Syria na Lebanon, al-Qaranah, Wadi al-Dar na Wadi al-Sahrij, yaliyoko katika miinuko ya al-Qalamun nchini Syria. Katika operesheni za kudhibiti maeneo hayo, makundi ya magaidi wa kundi la Jab’hatu Nusra, wakiwamo Abu Mujahid na al-Aswad, makamanda wa ngazi za juu wa kundi hilo, wameangamizwa na jeshi la nchi hiyo na wanamapambano wa Hizbullah ya Lebanon

No comments:

Post a Comment