Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 1 May 2015

Marekani yawapa magaidi wa Syria dola bilioni 3

Mkuu wa kundi linalojiita "Muungano wa Kitaifa wa Wapinzani wa Nje ya Syria" ameishukuru Marekani kwa kuyasaidia kifedha makundi ya waasi wa nchi hiyo na kuiomba iendelee kuwa pamoja na waasi hao kwa hali na mali.
Shirika la habari la Ufaransa limemnukuu Khaled Khoja akisema hayo jana wakati alipoona na John Kerry, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani na kuongeza kuwa, anaishukuru mno Marekani kwa kutoa msaada wa dola bilioni 3 kwa waasi wa Syria ambao uliwezesha kuanzishwa vita dhidi ya serikali ya Damascus.
Khaled Khoja ameongeza kuwa, waasi wa Syria wanaiomba Marekani iwasaidie kuzuia mashambulizi ya serikali ya Damascus ya kukomboa maeneo yanayodhibitiwa na waasi.
Mkuu huyo wa wapinzani wa Syria walioko nje ya nchi hiyo aidha amefumbia macho jinai zinazoendelea kufanywa na makundi ya kigaidi na uungaji mkono wa kila hali wa Marekani kwa makundi hayo ya kigaidi na kudai kuwa Rais Bashar al Assad hana uhalali wa kuwa Rais wa nchi hiyo licha ya wananchi wa Syria kumchagua kwa kura nyingi

No comments:

Post a Comment