Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 4 May 2015

Wakala wa Daesh atiwa nguvuni Lebanon

Magaidi wa Daesh Magaidi wa Daesh
Mwanachama wa ngazi ya juu wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh ametiwa mbaroni nchini Lebanon huku akiwa na pasi bandia ya kusafiria. Ibrahim al Barakat alitiwa mbaroni mapema jana na anatuhumiwa kwa kuwa wakala wa kundi la kigaidi la Daesh. Hayo yameelezwa na afisa usalama wa Lebanon. Barakat alitiwa mbaroni wakati alipokuwa akijaribu kuelekea Uturuki kupitia kaskazini mwa Lebanon huku akitumia pasipoti bandia.
Mbali na kuvishambulia vikosi vya Lebanon mwaka jana, Ibrahim al Barakat aliye na umri wa miaka 40 anakabiliwa na tuhuma za kuwasajili vijana kutoka Tripoli, mji mkubwa zaidi huko kaskazini mwa Lebanon, kwa ajili ya kupigana na wanamgambo huko Syria na Iraq. Tarehe 11 mwezi Oktoba mwaka jana, wanajeshi 11 wa Lebanon waliuliwa baada ya mapigano kuzuka kufuatia kutiwa mbaroni raia mmoja wa Lebanon aliyekuwa akituhumiwa kuwasajili vijana kujiunga na makundi ya kigaidi huko Syria.

No comments:

Post a Comment