Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 1 May 2015

UN yashindwa kudhibiti hali ya mambo nchini Libya

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa umoja huo umeshindwa kuyashawishi makundi hasimu nchini Libya kufanya mazungumzo baina yao. Mjumbe huo wa Umoja wa Mataifa nchini Libya ameyapa makundi ya Libya muda wa wiki moja yahakikishe kuwa yametangaza misimamo yao kuhusiana na muswada wa makubaliano ya amani yaliyopendekezwa na Umoja wa Mataifa. Bernardino Leon amesema kuwa, ana matumaini makubaliano hayo yataandaa mazingira mazuri ya kupatikana amani ya kudumu nchini Libya. Hata hivyo wanamgambo wa Fajr ambao wanaudhibiti mji mkuu Tripoli jana waliutaka Umoja wa Mataifa umuondoe mjumbe wake huyo nchini Libya. Aidha wanamgambo hao wamewataka wakazi wa Tripoli wajitokeze kwa wingi leo Ijumaa katika maandamano ya kupinga hatua ya Umoja wa Mataifa ya kuingilia mgogoro wa Libya. Kundi hilo pia limepinga waziwazi mwito wa Bernadino Leon, mwakilishi wa Umoja wa Mataifa nchini Libya wa kuyataka makundi hasimu yarejee kwenye meza ya mazungumzo ya amani. Mwezi Septemba mwaka 2014 Umoja wa Mataifa ulianza rasmi kupatanisha mgogoro wa Libya baina ya jeshi na wanamgambo wa nchi hiyo hata hivyo mapigano ya mara kwa mara yamekuwa yakikwamisha juhudi hizo za Umoja wa Mataifa.

No comments:

Post a Comment