Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 8 May 2015

Daesh wagawa madawa ya kulevya kwa vijana wa Iraq

Duru za habari kutoka Iraq, zimeripoti kuwa, kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh limekuwa likigawa madawa ya kulevya kwa vijana wa nchi hiyo ili kuwafanya waweze kujiunga na kundi hilo katika kutekeleza jinai za kigaidi. Hayo yamethibitishwa na Farhan Muhammad, kiongozi mwandamizi wa Baraza la Mkoa wa al-Anbar na kuongeza kuwa, baada ya kundi hilo la kigaidi linalotenda jinai kwa jina la Uislamu, kuingiza idadi kubwa ya madawa ya kulevya ya aina mbalimbali vikiwemo vidonge kupitia mipaka ya Syria kuelekea al-Anbar, wanachama wa Daesh, wamekuwa wakigawa madawa hayo ya kulevya kwa vijana wa mkoa huo kitendo kinachotajwa kuwa ni njia mojawapo ya kuweza kuwafanya vijana wengi wajiunge nalo. Kwa mujibu wa afisa huyo wa serikali, kundi la Daesh, linatekeleza mpango wa kuwatia kasumba vijana, sanjari na kuwatumia katika kutekeleza jinai zake hapo baadaye. Amewataka viongozi wa kundi hilo linalojinadi kuwa na mafungamano na Uislamu kutekeleza jukumu lao la kidini, badala ya kwenda kinyume na misingi ya dini hiyo tukufu inayopiga marufuku vitendo vya aina hiyo. Hayo yanajiri katika hali ambayo, hivi karibuni kulienea habari kwamba, wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh wamekuwa wakitumia vidonge vya kulevya ili kuwafanya wasipitiwe na usingizi vitani. Mbali na hapo hivi karibuni pia kundi hilo liliifanyia matengenezo hoteli ya kimataifa ya Nainawa iliyopo katika mji wa Mosul nchini Iraq ambayo itatumiwa na makamanda wake katika starehe na anasa. Mambo hayo pamoja na mengineyo, ndiyo yaliyowafanya weledi wa mambo waamini kuwa, kundi hilo kinyume na madai yake, linakwenda kinyume na misingi ya Kiislamu na linatekeleza njama za Wamagharibi dhidi ya dini hiyo tukufu

No comments:

Post a Comment