Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 11 May 2015

Wapinzani nchini Burundi waendelea kuandamana

Wapinzani nchini Burundi wamepuuza onyo la serikali la kupiga marufuku maandamano na badala yake wameendelea kuandamana wakipinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza ya kuogombea kwa muhula mwingine wakisisitiza kuwa, hatua hiyo inakinzana na Katiba na mkataba wa Arusha. Jana mamia ya wanawake waliandamana katika mji mkuu Bujumbura na kukusanyika katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo. Taarifa zaidi kutoka Burundi zinasema kuwa, mgogoro wa kisiasa unaoikabili nchi hiyo umezorotesha shughuli za kiuchumi. Jumuiya mbalimbali ukiwemo Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Afrika Mashariki zimeendelea kutoa wito wa kudumishwa amani na utulivu nchini humo.
Takribani watu 15 wamepoteza maisha katika ghasia na maandamano nchini Burundi. Wapinzani wanasema Nkurunziza anakiuka mapatano ya Arusha yaliyomaliza vita vya ndani nchini humo, lakini wafuasi wa rais huyo wanasema katika muhula wake wa kwanza Nkurunziza alichaguliwa na Bunge na hivyo muhula huo hauwezi kuhesabiwa.

No comments:

Post a Comment