Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 15 May 2015

Assad: Wasyria ni imara katika kupambana na ugaidi

Rais Assad akizungumza na ujumbe wa Iran mjini Damascus, Mei 13 2015 Rais Assad akizungumza na ujumbe wa Iran mjini Damascus, Mei 13 2015
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema magaidi hawatafanikiwa katika njama zao za kuvuruga azma ya Wasyria katika mapambano yao dhdi ya ugaidi.
Assad ameyasema hayo Jumatano mjini Damascus katika mkutano na Alaeddin Boroujerdi, Mkuu wa Kamati ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni katika Bunge la Iran, Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu.
Katika kikao hicho, Assad na Boroujerdi walijadili na kuashiria uungaji mkono wanaopata magaidi kutoka baadhi ya nchi za Magharibi na waitifaki wao katika eneo na kusema magaidi ni vibaraka wa nchi zinazowaunga mkono. Rais wa Syria amesema magaidi na waungaji mkono wao wamekuwa wakifanya hadaa na kueneza propaganda ili kufidia kipigo wanachopata katika medani ya vita. Amesema kwa irada yao imara na msaada wa nchi rafiki kama Iran, Wasyria wanaangamiza ugaidi na machafuko katika nchi yao. Kwa upande wake Boroujerdi amewapongeza Wasyria, jeshi na uongozi wa nchi hiyo kwa kusimama imara na kuongeza kuwa, wakiendelea hivyo hatimaye watapata ushindi kamili dhidi ya magaidi. Aidha amesema Iran itaendelea kuiunga mkono Syria hadi pale mgogoro utakapomalizika nchini humo. Wakati huo huo duru za habari zinasema wapiganaji wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon wamepata mafanikio makubwa katika mapamabano na magaidi katika milima ya Qalamoun kaskazini mwa Damascus

No comments:

Post a Comment