Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 24 May 2015

Daesh waua raia 400 katika mji wa Palmyra, Syria

Kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh limewaua kwa halaiki raia 400 wa Syria, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto katika shambulio dhidi ya mji wa kale na wa kihistoria wa nchi hiyo wa Palmyra. Televisheni ya Syria imeripoti jinai hiyo iliyofanywa na magaidi hao wanaoungwa mkono na madola ya kigeni ikiwanukuu wakaazi wa mji huo wa kihistoria wenye magofu ya kale yaliyohifadhiwa vizuri ya tokea enzi za utawala wa Rumi yakiwemo mahekalu. Mauaji hayo ya halaiki yamefanywa na magaidi wa kundi la Daesh baada ya kuwatuhumu wakaazi wa mji wa Palmyra kuwa wanashirikiana na serikali na kukataa kutii amri za magaidi hao. Wakati huohuo wanaharakati wa upinzani wameeleza kupitia mitandao ya kijamii kuwa mamia ya miili ilikuwa imetapakaa barabarani katika mji huo baada ya kushikiliwa na kundi la kitakfiri la Daesh siku ya Jumatano iliyopita. Katika upande mwengine Mkurugenzi wa Mambo ya Kale wa serikali ya Syria Mamoun Abdulkarim amesema athari nyingi za kihistoria zilizokuwemo kwenye makumbusho ya mji wa Palmyra zimeondolewa, lakini imeshindikana kuzihamisha baadhi ya nyengine zenye uzito wa tani tatu hadi nne. Itakumbukwa kuwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh ni maarufu kwa ubomoaji wa maeneo ya turathi za kihistoria kwa madai kwamba athari hizo ni nembo na alama za shirk

No comments:

Post a Comment