Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 4 May 2015

Hamas ipo tayari kushiriki uchaguzi Palestina

Wafuasi wa Hamas Wafuasi wa Hamas
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imetangaza kuwa ipo tayari kushiriki katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa bunge na urais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina. Hamas imetoa taarifa na kutangaza utaarifu wake kwa ajili ya kushiriki katika uchaguzi wa Palestina na kumtuhumu Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina kuwa ndiye anayekwamisha utekelezaji wa mchakato wa kisheria wa uchaguzi. Taarifa ya Hamas imeongeza kuwa Mahmoud Abbas halipi uzito wa hali ya juu suala la kufanyika uchaguzi na anakwamisha kuainishwa tarehe ya kufanyika chaguzi hizo. Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas vile vile imeshutumu matamashi ya Mahmoud Abbas kwamba upo ulazima kwa Hamas kuwasilisha ombi la kimaandishi kwa ajili ya kufanyika uchaguzi huo na kuongeza kuwa matamshi hayo ni wazi yatazidisha mgawanyiko kati ya Wapalestina na kukwamisha kufikiwa makubaliano na mapatano ya kitaifa.

No comments:

Post a Comment