Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 8 May 2015

Wanigeria waliokuwa Niger walazamika kurudi makwao

Maelfu ya raia wa Nigeria waliokimbia mashambulizi ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram, wamefukuzwa nchini Niger. Taarifa iliyotolewa leo na kiongozi mmoja wa Niger, imesema kuwa, zaidi ya watu elfu tatu miongoni mwa wavuvi na wakimbizi raia wa Nigeria ambao walikimbia nchi yao kutokana na mashambulio ya kundi hilo, tayari wameondoshwa nchini humo. Kwa upande wao raia hao wa Nigeria, wamenukuliwa wakisema kuwa, wamelazimika kurejea nchini mwao na kwamba mamia ya wakimbizi wengine wa nchi hiyo nao wanajiandaa kurudi makwao. Wameongeza kuwa, watu watatu kati yao walipoteza maisha kutokana na kutembea kwa muda mrefu usiopungua siku tatu katika safari hiyo ya kurejea kwao. Kufuatia taarifa hiyo, serikali ya Nigeria, imeahidi kupeleka malori kwa ajili ya kuwabebea wakimbizi hazo. Charles Otegbabe, mmoja wa maafisa wa serikali ya Nigeria amethibitisha habari hiyo na kusema kuwa, serikali imewapokea wakazi wa mji wa Gaidam, uliopo katika jimbo la Borno ambao awali walikimbilia nchini Niger ili kuokoa maisha yao kipindi kundi la Boko Haram liliposhadidisha jinai zake nchini humo. Kwa mujibu wa serikali ya Niger,  Jumatatu iliyopita, jeshi la nchi hiyo lilitekeleza operesheni katika eneo la ziwa Chad nchini humo na kuchukua hatua ya kuwahamisha raia kutoka sehemu moja kwenda nyengine . Hii ni katika hali ambayo Niger, imewapa hifadhi raia wapatao laki moja wa Nigeria waliokimbilia nchini humo kuokoa maisha yao kutokana na mashambulizi ya kundi la Boko Haram.

No comments:

Post a Comment