Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 15 May 2015

Saudia yavunja mapatano ya usitishaji vita Yemen

Watu wasiopungua tisa wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya ndege za kivita za Saudia kudondosha mabomu licha ya utawala huo wa Riyadh kutangaza usitishaji wa hujuma yake ya kijeshi ya wiki saba dhidi ya nchi hiyo masikini.
Duru zinaarifu kuwa Wayemen kadhaa wameuawa leo baada ya ndege ya helikopta aina ya Apache kushambulia eneo la al-Safiya katika mkoa wa Sa'ada kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Hali kadhalika mapema leo ndege za kivita za Saudia zimedondosha mabomu katika bandari ya Aden na mikoa ya Hajjah na Abyan. Saudia imekiuka tangazo lake la usitishaji vita kwa muda wa siku tano kuanzia Jumanne. Wakati huo huo Iran imesema meli yake inayopelekea misaada ya kibinadamu Yemen imefanya hivyo kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya Kiafrika na Kiarabu Hossein Amir-Abdollahian amesisitiza kuwa meli hiyo ya misaada ya Iran itafika Yemen kama ilivyopangwa. Hivi karibuni Kamanda mwandamizi wa jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alitahadharisha kuwa, shambulizi lolote dhidi ya meli ya misaada ya kibinadamu ya Iran inayoelekea Yemen litawasha moto wa vita katika eneo zima la Mashariki ya Kati. Jenerali Masoud Jazayeri, amesema meli hiyo iliyopewa jina la 'Nejat' yaani 'uokovu' imebeba misaada ya kibinadamu kama vile chakula na dawa na wala haipaswi kuzuiwa au kushambuliwa kwa mujibu wa sheria za kimataifa

No comments:

Post a Comment