Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 1 May 2015

Ban asikitishwa na jinai za Saudia nchini Yemen

Ban Ki moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa anasikitishwa na hatua ya Saudi Arabia ya kuendeleza mashambulizi nchini Yemen.
Ban alisema hayo jana na kuongeza kuwa, mashambulizi dhidi ya raia na miundombinu isiyo ya kijeshi zikiwemo hospitali na maeneo ya Umoja wa Mataifa nchini Yemen hayakubaliki kabisa na ni uvunjaji wa wazi wa haki za binadamu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametosheka tu na kusema anasikitishwa na jinai hizo za Saudi Arabia nchini Yemen katika hali ambayo mashambulizi dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu yameendelea kusababisha maafa kwa watu wasio na hatia.
Karibu watu 1,000 wameshauwa katika mashambulizi ya Saudia nchini Yemen wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto wadogo.
Jana pia ndege za Saudi Arabia zilishambulia ofisi za televisheni ya al Masirah ambayo inahesabiwa kuwa marejeo makubwa ya habari zinazohusiana na mashambulizi ya Saudia nchini Yemen

No comments:

Post a Comment