Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 4 May 2015

Watu waliovalia sare za jeshi waua makumi Nigeria

Watu waliokuwa na silaha wameuwa makumi ya raia, wengi wao wakiwa wanawake na watoto huko Nigeria katika mfululizo wa mashambulizi dhidi ya vijiji kadhaa katika jimbo la Plateau. Nanzing Bani kiongozi wa jamii katika eneo amesema kuwa mauaji hayo yalitokea jana wakati watu waliokuwa na silaha huku wakiwa wamevalia sera za kijeshi walifanya ufyatuaji risasi wa kiholela dhidi ya raia huko katika eneo la Kardarko na katika vijiji jirani jimboni Plateau. Kiongozi huyo wa kieneo amesema kwamba idadi ya waliouawa inaweza kufikia 100. Watu walioshuhudia na wenyeji wa eneo hilo wamesema kuwa wavamizi walichoma moto majengo na nyumba nyingi katika eneo hilo. Mashambulizi hayo ya watu wenye silaha yamepelekea makumi ya wakazi wa eneo hilo la katika jimbo la Plateau kuzihama nyumba zao.

No comments:

Post a Comment