Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 12 May 2015

Jeshi la Iraq laua wanamgambo 73 wa kundi la Daesh

Uongozi wa operesheni za kijeshi za Dijla nchini Iraq umetangaza kuwa, vikosi vya nchi hiyo vimefanikiwa kukomboa kikamilifu kisima cha mafuta cha Ajil, mashariki mwa mji wa Tikrit baada ya kupambana vikali na wanamgambo wa kundi la kigaidi la Daesh na kuua wanamgambo 73.
Vyombo vya habari vya Iraq vimemnukuu Luteni Jenerali Abdul Amir al Zaydi akisema kuwa, mapigano makali yalizuka baina ya vikosi vya Iraq na wanamgambo wa Daesh na kupelekea wanamgambo 73 kuuawa wakiwemo wenye uraia wa kigeni.
Luteni Jenerali al Zaydi ameongeza kuwa, askari watatu wa vikosi vya ulinzi vya Iraq wameuawa na wengine 13 kujeruhiwa katika mapambano hayo.
Vikosi vya ulinzi vya Iraq vimefanikiwa pia kuangamiza magari 37 ya kivita ya kundi la kigaidi la Daesh.
Ameongeza kuwa, kisima hicho cha mafuta kilichovamiwa na wanamgambo wa Daesh kinadhibitiwa kikamilifu na vikosi vya ulinzi vya Iraq hivi sasa

No comments:

Post a Comment