Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amelaani mauaji ya
kiongozi wa upinzani nchini Burundi. Zedi Feruzi, kiongozi wa chama cha
Umoja kwa ajili ya Amani na Maendeleo ya Burundi (UPD-Zigamibanga)
aliuliwa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana jana usiku wakati
alipokuwa akielekea nyumbani kwake katika wilaya ya Ngagara iliyoko
katika mji mkuu wa nchi hiyo Bujumbura. Taarifa iliyotolewa na Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa kupitia msemaji wake imeeleza kuwa jinai hiyo
na ya shambulio la guruneti la siku ya Ijumaa katika soko kuu la jiji la
Bujumbura lililoua watu wawili na kujeruhi wengine wengi yanatishia
kuleta hali ya kutoaminiana na kuchochea machafuko nchini humo. Ban
Ki-moon amewahimiza wadau mbalimbali nchini Burundi kufuatilia
mazungumzo ya kisiasa yaliyoandaliwa na Umoja wa Mataifa na kuhusisha
wawakilishi wa serikali, vyama vya upinzani na jumuiya za kidini.
Wakati huohuo wanaharakati wa upinzani nchini Burundi wamesimamisha mazungumzo na serikali kufuatia mauaji ya kiongozi wa chama cha upinzani cha UPD-Zigamibanga. Katika taarifa yao waliyoitoa mapema leo, wanaharakati hao wamelaani mauaji hayo waliyoeleza kuwa ni "kitendo kibaya sana" na kusema, wanasimamisha mpango wa kufanya mazungumzo na serikali. Aidha wamesema mauaji ya Zedi Feruzi yanaweza yakawa sehemu ya mpango wa kuwaondoa viongozi wanaoendesha kampeni dhidi ya Rais Pierre Nkurunziza wa nchi hiyo. Watu wapato 30 wameshauawa hadi sasa nchini Burundi katika matukio mbalimbali yakiwemo ya mashambulio na mapigano kati ya polisi na waandamanaji wanaopinga uamuzi wa Nkurunziza wa kugombea urais kwa muhula wa tatu
Wakati huohuo wanaharakati wa upinzani nchini Burundi wamesimamisha mazungumzo na serikali kufuatia mauaji ya kiongozi wa chama cha upinzani cha UPD-Zigamibanga. Katika taarifa yao waliyoitoa mapema leo, wanaharakati hao wamelaani mauaji hayo waliyoeleza kuwa ni "kitendo kibaya sana" na kusema, wanasimamisha mpango wa kufanya mazungumzo na serikali. Aidha wamesema mauaji ya Zedi Feruzi yanaweza yakawa sehemu ya mpango wa kuwaondoa viongozi wanaoendesha kampeni dhidi ya Rais Pierre Nkurunziza wa nchi hiyo. Watu wapato 30 wameshauawa hadi sasa nchini Burundi katika matukio mbalimbali yakiwemo ya mashambulio na mapigano kati ya polisi na waandamanaji wanaopinga uamuzi wa Nkurunziza wa kugombea urais kwa muhula wa tatu
No comments:
Post a Comment