Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 12 May 2015

Televisheni ya al Masirah yaonesha ndege ya Morocco

Mabaki ya ndege ya kijeshi ya Morocco iliyotunguliwa na wanamapambano wa kikabila wa Yemen Mabaki ya ndege ya kijeshi ya Morocco iliyotunguliwa na wanamapambano wa kikabila wa Yemen
Televisheni ya al Masirah ya nchini Yemen imerusha hewani mkanda wa video unaoonesha ndege yenye bendera ya Morocco iliyoangushwa na wanamapambano wa kikabila wa Yemen kaskazini mwa nchi hiyo. Katika mkanda huo wa video, anaonekana mwandishi wa televisheni hiyo akionesha baadhi ya mabaki ya ndege hivyo ambapo katika sehemu moja ya mabaki hayo ya ndege kunaonekana pia bawa la ndege lenye bendera ya Morocco. Wapiganaji wa kikabila wanaonekana wakishingiria na kukusanya mabaki ya ndege hiyo ya kijeshi ya Morocco aina ya F16 iliyokuwa inafanya mashambulizi dhidi ya wananchi wa Yemen. Huku hayo yakiripotiwa, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya Afrika na Kiarabu, Hussein Amir Abdollahiyan amesema kuwa kinachotarajiwa kutoka kwa Umoja wa Mataifa ni kuchukua hatua za maana za kukomesha uadui wa Saudi Arabia dhidi ya wananchi wa Yemen. Bw. Abdollahiyan alisisitiza hayo katika mazungumzo ya simu baina yake na mjumbe mpya wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika kadhia ya Yemen, Bw. Ismail Ould Cheikh

No comments:

Post a Comment