Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 12 May 2015

Pakistan yatuma askari usalama nchini Bahrain

Viongozi wa Pakistan wametangaza kuwa wametuma askari maalumu wa masuala ya kiusalama nchini Bahrain baada ya kuombwa na viongozi wa ukoo wa kifalme wa Aal Khalifa ili kupambana na wimbi la mapinduzi la wananchi wa nchi hiyo. Shirika la habari la Reuters limezinukuu duru za Pakistan zikifichua jana kuwa, askari maalumu wa masuala ya kiusalama wa Pakistan wametumwa nchini Bahrain ili kushirikiana na mamluki kutoka nchi nyinginezo kwa ajili ya kuzima harakati za kimapinduzi za wananchi wa nchi hiyo. Hayo yameripotiwa katika hali ambayo wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaamini kuwa, si jambo rahisi kuweza kuzimwa harakati hizo za wananchi wa Bahrain hasa kutokana na kuwa, Saudia ambayo imetuma wanajeshi wake kukandamiza wananchi wa Bahrain, hivi sasa inafanya jinai pia katika nchi nyingine ya Kiarabu na Kiislamu ya Yemen. Vile vile utawala wa kifalme wa Bahrain unaendelea kumshikilia Sheikh Ali Salman, Katibu Mkuu wa chama cha Kiislamu cha al Wifaq cha nchi hiyo pamoja na Nabil Rajab, mwanaharati wa haki za binadamu wa Bahrain. Utawala wa ukoo wa Aal Khalifa huko Bahrain umeomba msaada kutoka kwa Marekani, Saudi Arabia na baadhi ya nchi kama vile Pakistan ili kuzima harakati za wananchi wa nchi hiyo wanaopigania haki zao na kuupinga utawala huo wa kiimla

No comments:

Post a Comment