Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 1 May 2015

Kiongozi wa waasi wa ADF atiwa mbaroni nchini TZ

Habari kutoka nchini Tanzania zinasema kuwa, kiongozi wa kundi la waasi wa ADF wa nchini Uganda ametiwa mbaroni nchini Tanzania. Vyombo vya habari yakiwemo magazeti ya nchini Uganda yamethibitisha kutiwa mbaroni mtu anayeaminiwa kuwa ni Jamil Mukulu, mkuu wa kundi la waasi wa ADF ambao wanatuhumiwa kufanya mauaji ya watu 300 tangu mwezi Oktoba hadi hivi sasa katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Habari zinasema kuwa Mukulu ametiwa mbaroni kwa ushirikiano wa polisi wa Tanzania na wenzao wa Uganda. Hata hivyo jeshi la Uganda limesema kuwa haliwezi kuthibitisha kuwa mtu aliyetiwa mbaroni ni Jamil Mukulu hadi atakapochukuliwa vipimo vya vinasaba, DNA. Kwa muda mrefu polisi ya Uganda ilikuwa imetoa amri ya kutiwa mbaroni kiongozi huyo wa waasi wa ADF mwenye umri wa miaka 51 kwa tuhuma za kufanya mauaji ya kigaidi na kuiomba Interpol iisaidie kutiwa mbaroni kiongozi huyo wa waasi. Kundi la ADF lilianzishwa mwaka 1995 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ili kupambana na siasa za Rais Yoweri Museveni wa Uganda

No comments:

Post a Comment