Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 24 May 2015

Saudia yalazimika kutangaza hali ya hatari mpakani

Saudi Arabia leo imelazimika kutangaza hali ya hatari katika ukanda wa mpaka wake wa kusini na Yemen baada ya kuongezeka mashambulizi ya makombora ya wanamapambano wa Yemen dhidi ya Saudia.
Televisheni ya al Masirah imetangaza kuwa, jeshi la Yemen na wapiganaji wa kamati za wananchi wa nchi hiyo wameendelea kushambulia maeneo ya Saudia yanayopakana na mkoa wa Saada, kama ambavyo wameshambulia kwa makombora pia jengo la walinzi wa mpakani wa Saudia katika eneo la at Twiwaal huko Jizan.
Wakati huo huo wakazi wa mkoa wa al Jawf wa kaskazini mwa Yemen wameandamana kulalamikia uongo unaoenezwa na televisheni za al Jazeera na al Arabiya. Televisheni ya al Masirah imeripoti kuwa, wananchi wa Yemen leo wameandamana katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa mpakani wa al Jawf kaskazini mwa Yemen wakikanusha na kulalamikia uongo unaonezwa na televisheni hizo za Qatar na Saudia kwamba eti wakazi wa mkoa huo wako tayari kupambana na Ansarullah. Waandamanaji wamesema kuwa, uongo kama huo hautatia doa mshikamano wa wananchi wote wa Yemen katika kukabiliana na jinai wanazofanyiwa na Saudia na waitifaki wake

No comments:

Post a Comment