Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 8 May 2015

Mwanachama wa Al Shabab ajisalimisha Kenya

Serikali ya Kenya, imetangaza kuwa mwanachama mmoja wa kundi la kigaidi la ash-Shabab nchini Somalia amejisalimisha kwa jeshi la polisi huko mkoani Garissa, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Kwa mujibu wa duru za usalama nchini humo, mwanachama huyo wa kundi hilo ambalo limekuwa likitekeleza jinai katika siku za hivi karibuni, amejisalimisha kwa polisi ya Kenya baada ya kujiengua kutoka kundi hilo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, gaidi huyo wa ash-Shabab ambaye bado hajatajwa jina lake, amechukua uamzi huo kulalamikia jinai ambazo zimekuwa zikitekelezwa na wanachama wa kundi hilo dhidi ya watu wasio na hatia katika maeneo tofauti ya ndani na nje ya Somalia. Inaelezwa kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 22, ambaye hajatajwa kwa sababu za kiusalama, alijiunga na kundi hilo hapo mwaka 2011. Amesema kuwa, amejisalimisha kwa jeshi la serikali kupitia fremu ya msamaha uliotangazwa na serikali ya Nairobi kwa wanachama wa kundi hilo. Kwengineko viongozi wa serikali ya Nairobi wametangaza kuwa, makumi ya vijana waliokuwa wamejiunga na kundi hilo la kigaidi, wamerejea makwao kufuatia operesheni za askari wa kusimamia amani wa Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM. Mwanzoni mwa mwaka huu, serikali ya Kenya ilitangaza msamaha kwa wote kwa ajili ya vijana waliojiunga na kundi la kigaidi la ash-Shabab.

No comments:

Post a Comment