Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 12 May 2015

Saudia yashirikiana kijasusi na utawala wa Kizayuni

Ndege ya Saudi Arabia ikiwa katika Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion huko Tel Aviv. Ndege ya Saudi Arabia ikiwa katika Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion huko Tel Aviv.
Duru za kuaminika zimefichua kuwa, Saudi Arabia na utawala wa Kizayuni wa Israel zimetiliana saini mkataba wa ushirikiano wa kijasusi katika suala la Yemen pamoja na kutumiwa ndege zisizo na rubani za Kizayuni katika anga ya Yemen. Mwandishi wa Radio Tehran amezinukuu duru za kuaminika zikifichua kuwa, Khalid bin Ali bin Abdullah al Hamidan, mkuu wa shirika la kijasusi la Saudi Arabia hivi karibuni alielekea katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni na kutia saini mkataba wa ushirikiano wa kijasusi kati ya Saudia na utawala wa Kizayuni wa Israel. Kabla ya hapo baadhi ya vyombo vya habari kama vile televisheni ya al Alam na gazeti la Kizayuni la Yediot Ahronot vilitangaza habari ya kutua ndege ya Saudi Arabia katika uwanja wa ndege wa Ben-Gurion huko Tel Aviv. Mashirika ya habari yalisema kuwa ndege hiyo ilikuwa ya mwana mmoja wa ukoo wa kifalme wa Aal Saud ingawa Saudia ilidai kuwa ndege hiyo ilikuwa na shirika la ndege la Ureno. Hii si mara ya kwanza kuripotiwa habari za ushirikiano baina ya utawala wa Kizayuni wa Israel na ukoo wa Aal Saud na habari za kuweko ushirikiano mpya baina ya pande hizo mbili dhidi ya wananchi wa Yemen zinatilia nguvu ushirikiano wa muda mrefu baina ya Saudia na utawala wa Kizayuni wa Israel.

No comments:

Post a Comment