WAMEAMINISHWA KUWA ADUI YAO NI KILA MTETEA ZANZIBAR.Kwao wao huyu ni hatari zaidi kuliko mkoloni, wameshatengenezwa kukubali utumwa. Mpaka lini haya? Aje nani tena atwambie umuhimu wa kuwa na nchi yetu huru na maamuzi ili watawala watanabahi? nani aje? kama ni viongozi wazalendo wote walikwenda na maji, kama ni wanavindaki ndaki wameshikishwa adabu, kama ni wapinzani wameshakubuhu hakuna jipya. Kimebaki nini tena? si tulibadilisha Katiba na kutamka sasa Zanzibar ni nchi imekuwaje? wachumia tumbo walijivisha gunia la usaliti na kujifunga vibwebwe viunoni na kukata viuno kule DODOMA. Walisherehekea UTUMWA wa milele kwa pipi ya Sukari zamani ikiitwa FAGI.Ili Zanzibar ibaki kuwa koloni. Sherehe ile ilikuwa na maana moja kubwa. KUKUBALI KUWA WATUMWA WA MILELE. Haingii akilini Kwamba ni juzi tu Mwanakindaki ndaki kipenzi chetu kutumia wadhifa wake na kujitowa muhanga kuirejesha Zanzibar katika nafasi yake eti leo amekuwa ADUI wa Wachumia tumbo. Hawa walikuwa nae bega kwa bega na walijivisha kilemba cha ukoka kuwa wako pamoja nae ili Zanzibar irudi kwenye heshima. Wapi leo. Genetics zimewazidi nguvu wamerudi katika uhalisia wao.
Bahati mbaya sana MILAFI imetuzuwiya kutumia fursa ya kihistoria pale ambapo mkoloni wetu mara hii alifurahi na kucheka na kusema hebu semeni mnataka nini badala ya kusema tunataka uhuru basi mitawala yetu ilisema tunataka KUTAWALIWA na KUWA WATUMWA WA MILELE.Ilitumia hilba yao kama kawaida kuziba sauti za Wazanzibari na kujifanya wasemaji wetu. Mbona kama ni wema hawatuulizi kupitia maoni huru tunataka nini. Wapi? fursa haiji mara mbili. Nasikitika na wale wanaoishabikia MITAWALA HII. Hawa kama ingekuwa ni katika uhalifu na wao wangekuwa wasaidia uhalifu.Wanapaswa kuadhibiwa kama walivyo wahalifu wengine lakini tuseme bado wakati wao ingawa hauko mbali.
Wamesahau awamu zote zikipiga kelele na safari iliishia njiani, awamu ya sita ilitenda na kuthubutu kuweka mazingira yote ya kurejea kwa Zanzibar. Hatimae nafasi ya mtende ikaja. Damu ya wasaliti ikachemka wakasahau kilio chao cha kama miezi mitano walipotowa machozi YA MAMBA YA KUITETEA Zanzibar katika Tume ya KATIBA. Hawachoki na wala hawashibi. Usaliti una lana kama ulivyo ulevi. Toka lini mtu kuvimbiwa pipi kama si uroho tu. Zanzibar imepotezwa kwa mikono ya wasaliti hawa na sasa miaka hamsini wanataka TUWAAMINI tena kwa lipi jipya? au mafuta ya mgando kungarisha kiatu?
Hatutawasamehe daima mpaka mtubu.Mnatuchagulia utumwa badala ya uhuru halafu mnataka tuwaunge mkono. Kamwe hatutafanya hivyo. Nyinyi endeleeni na shari zenu na hilba kama kawaida. Ni bora mshinde kwa HADAA MKIWA PEKEYENU MTAUSEMA UKWELI MCHUNGU JAPO VYOONI KWAMBA Wazanzibari WAMETUKATAA TENA. ENDELEENI TU.
Baya zaidi sasa mnazidi na mnakaribia laana ya wazi. Hili la kuwaadhibu na kuwafungulia kesi za kizushi mashehe si jema kwa mustkabali wa nchi. Mmeshavuka mipaka sasa subirini gharika itakayosababishwa na mikono yenu. Msije mkatafuta wachawi. Mnajuwa mipango ilisukwa na nani na kila mmoja atawajibika kivyake wakati ukifika.Wote safari yetu ni moja.Lakini hili la kuwaadhibu masheikh nawasihi mnakwenda KOMBO ZAIDI.Yaani mnajikubalisha utumwa mpaka kuwauza raia wenu ili nyinyi muishi na kuwapendezesha wakoloni kiasi cha kukosa utu. Hebu fikirini wale watoto wa masheikh wamekosa mangapi kwa maamuzi yenu yasiyo na uzalendo? Mmeekubali utumwa mpaka kwa mambo yasiyostahiki.
Hizi sio zama za kawaida. Nawasihi Wazanzibari kwa umoja wetu tujali UZALENDO. Kumeletwa misingi ya kidemokrasia katika kuonesha hisia na kuleta mabadiliko ya kiutawala KATIKA NCHI. MARA HII NI ZADI YA SIASA ZA VYAMA. Tusipoziba ufa tutajenga ukuta. Hata niandike vitabu mia sitomaliza kuonesha UCHOVU wa watawala wetu ingawa wenyewe wanakataa kuwa hivyo.
Mpaka lini tutaendelea kulalamika, kupumbazwa, kughilibiwa na kutumiwa kufanikisha mipango miovu dhidi ya MUSTAKABALI WA ZANZIBAR? Mpaka lini tutasemewa tusiyoyataka? aje nani afashamishe hili kuwa Zanzibar imepotezwa na Watawala wetu kwa miaka zaidi ya hamsini sasa? Inasikitisha kuona watawala wakati mwengine wanalia na kulalamika eti tusimame kwa MIGUU YETU sasa? hawa si ndio waliopiga kelele za furaha na kukata mauno kule Dodoma? mna mlilia nani?
MATUMAINI YA MABADILIKO KWA KUTUMIA MAARIFA YOTE YANAPASWA KUELEKEZWA KUWAZIBA SAUTI WASALITI KATIKA MAAMUZI YA KURA.
TUKATAE KUCHAGULIWA UTUMWA, TUWAKATAE WOTE WANAOTUTIA UTUMWANI.
MUNGU IBARIKI ZANZIBAR