Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 12 December 2014

Ansarullah ya Yemen yapinga mpango wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi

Nchi wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (PGCC) ambazo mwaka 2011 ziliingilia kati mgogoro wa Yemen na kuzuia mapinduzi ya wananchi wa nchi hiyo kupata ushindi, kwa mara nyengine tena, hivi sasa zinafanya kila njia ili kuzima tena wimbi la mabadiliko ya kisiasa lililoanza nchini humo tangu mwezi Julai mwaka huu. Katika taarifa iliyotolewa mwishoni mwa kikao cha 35 cha Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kilichofanyika siku ya Jumanne katika mji mkuu wa Qatar, Doha nchi wanachama wa PGCC zimetaka wapiganaji wa Kihouthi wa Kamati za Wananchi waondoke katika mji mkuu wa Yemen, Sana’a na katika maeneo mengine yanayodhibitiwa na wapiganaji hao.
Ali Abdullah Saleh, ambaye kuanzia mwaka 1978 hadi 1990 alikuwa Rais wa Yemen ya Kaskazini, na kuanzia mwaka 1990 hadi mwaka 2011 alikuwa Rais pia wa Yemen iliyoungana, kama ilivyokuwa kwa watawala wa aghalabu ya nchi za Kiarabu za Mashariki ya Kati na za kaskazini mwa Afrika, mwaka 2011 naye pia alikabiliwa na wimbi kubwa la upinzani wa wananchi. Japokuwa Saleh alijaribu kuzima wimbi hilo la upinzani ili aweze kuendelea kubakia madarakani, lakini wananchi wa Yemen walishikilia msimamo wao kuhakikisha dikteta huyo anang’atuka madarakani. Licha ya hatua alizochukua Ali Abdullah Saleh mwenyewe, baadhi ya watawala wa nchi za Kiarabu za eneo, nao pia walijaribu kufanya juu chini ili kumwokoa dikteta huyo na gharika ya mapinduzi ya wananchi wa Yemen. Baadhi ya nchi wanachama wa PGCC na hasa Saudi Arabia ilikuwa moja ya viranja wakuu wa kumlinda Saleh na kuhakikisha anaendelea kushika hatamu za utawala, lakini nguvu na ukubwa wa wimbi la upinzani wa wananchi dhidi ya dikteta huyo, ziliulazimisha utawala wa kifalme wa Aal Saud ufikirie mbinu na hila nyengine kupitia PGCC ili kupotosha mkondo wa mapinduzi ya wananchi wa Yemen. Kulingana na mpango huo Ali Abdullah Saleh aling’atuka madarakani kwa sharti la kutoshtakiwa na kufatiliwa kisheria kwa jinai alizotenda, na akakabidhi madaraka kwa makamu wake Abd Rabbuh Mansur Hadi, kupitia uchaguzi wa kimaonyesho uliofanyika nchini humo. Mbinu na hila ya mpango wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi ulipotosha mkondo wa mapinduzi ya wananchi wa Yemen na kuwatumbukiza wananchi hao kwenye lindi la hali ya mchafukoge wa kisiasa iliyoendelea kwa muda wa miaka mitatu. Kushadidi hali hiyo na udhaifu mkubwa wa kiutendaji ulioonyeshwa na serikali ya mpito ya Abd Rabbuh Mansur Hadi, viliwafanya wananchi, wakiongozwa na harakati ya Mahouthi ya Ansarullah waanzishe wimbi jipya la maandamano dhidi ya serikali hiyo. Kushadidi na kuendelea wimbi hilo la maandamano ya upinzani lililoanza mwezi Julai mwaka huu hatimaye kuliipigisha magoti serikali ya Mansur Hadi, ambapo mnamo mwezi Septemba ilikubaliana na matakwa ya wananchi likiwemo la kujiuzulu serikali na kuundwa serikali mpya kwa maafikiano na harakati ya Ansarullah. Hata hivyo maafikiano hayo hayakukubaliwa na baadhi ya nchi wanachama wa PGCC hususan Saudi Arabia na Imarati. Kwa mtazamo wa Saudia, kuundwa serikali itakayotoa nafasi kuu kwa Ansarullah na kuifanya harakati hiyo iwe na sauti kubwa katika matukio ya Yemen ni tishio dhidi ya mipaka yake na pia kunaitia hofu na wasiwasi Riyadh juu ya kujitokeza mlingano mpya wa nguvu katika eneo. Wapinzani wa Ansarullah katika eneo wanaitakidi kuwa kupata nguvu harakati hiyo ambayo waungaji mkono wake waliowengi ni Mashia wa Zaidiyyah kutazipa nguvu zaidi harakati nyengine za kupinga tawala za kifalme katika nchi nyengine za Kiarabu na kuongezeka satua na ushawishi wa Iran nchini Yemen. Kwa sababu hiyo nchi wanachama wa PGCC zimetoa wito katika kikao chao cha 35 wa kutaka makubaliano ya Septemba yabatilishwe na wapiganaji wa Ansarullah waondoke katika mji mkuu wa Yemen na katika maeneo mengine wanayoyadhibiti. Baadhi ya viongozi wa harakati ya Ansarullah akiwemo Ali al Bukhaiti, mjumbe wa baraza la kisiasa na Hussein al Azi, mkuu wa mahusiano ya nje katika ofisi ya kisiasa ya harakati hiyo wamepinga azimio au taarifa yoyote ya kuingilia masuala ya ndani ya Yemen na kusisitiza kwamba taarifa ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi ni ya uingiliaji, ni tusi kwa wananchi wa Yemen na ni njama ya kushadidisha hitilafu za kimatapo na kimadhehebu katika nchi hiyo…/

No comments:

Post a Comment