Basi lililokuwa limewabeba wanajeshi wa Afghanistan
limeshambuliwa na mlipuaji wa kujitolea kufa viungani mwa mji mkuu,
Kabul, ambapo wanajeshi 6 wameuawa na wengine 11 kujeruhiwa. Dawlat
Waziri, afisa mwandamizi katika Wizara ya Ulinzi ya Afghanistan amesema
mlipuaji huyo wa kujitolea kufa alikuwa akitembea kwa miguu wakati
alipojilipua karibu na basi hilo leo mchana. Kundi la kigaidi la Taliban
limedai kuhusika na shambulizi hilo na limesema wanajeshi waliouawa ni
12 na kwamba wengine 13 wamejeruhiwa. Kundi la Taliban pia limedai
kuhusika na shambulizi jingine la leo asubuhi dhidi ya soko la umma
katika mkoa wa Herat ulioko magharibi mwa Afghanisan. Serikali haijataja
idadi ya waliouawa katika shambulizi hilo.
Katika wiki za hivi karibuni kundi la Taliban limeshadidisha mashambulizi dhidi ya majengo ya serikali, hoteli zinazotumiwa na raia wa kigeni pamoja na vituo vya polisi na jeshi ndani na nje ya mji wa Kabul.
Katika wiki za hivi karibuni kundi la Taliban limeshadidisha mashambulizi dhidi ya majengo ya serikali, hoteli zinazotumiwa na raia wa kigeni pamoja na vituo vya polisi na jeshi ndani na nje ya mji wa Kabul.
No comments:
Post a Comment