Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 19 December 2014

Kikwete atakiwa kuwachukulia hatua wahusika Escrow

Mashirika ya kigeni pamoja na nchi wafadhili wa Tanzania zimemtaka Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa nchi hiyo kuwachukulia hatua maafisa waandamizi wa serikali waliotajwa kuhusika na kashfa ya wizi ya Escrow.
Baadhi ya nchi zimetishia kusitisha misaada yao kwa Tanzania hadi pale kadhia hiyo itakapotatuliwa na wahusika kuwajibishwa. Marekani ambayo ni moja ya nchi wafadhili imetahadharisha kuwa itazuia msaada wa dola milioni 700 ambazo ni sawa na shilingi trilioni 1.1 za Tanzania kutokana na kashfa ya Tegeta Escrow.
Marekani imesema, mkataba wa pili wa miradi inayofadhiliwa na shirika la nchi hiyo la Changamoto za Milenia (MCC) utategemea hatua zitakazochukuliwa na serikali ya Tanzania dhidi ya wahusika wa kashfa hiyo.
Hayo yanajiri wakati Rais Jakaya Kikwete akisubiriwa kutoa maamuzi ya mapendekezo yaliyofikiwa na Bunge kuhusiana na sakata la wizi wa fedha zaidi ya Sh. bilioni 300 kutoka akaunti ya Tegeta Escrow wiki ijayo.
Baadhi ya nchi za Ulaya pia zimemtaka Rais Kikwete kuchukua hatua za haraka dhidi ya wahusika wa kashfa hiyo ya ufisadi la sivyo misaada kwa Tanzania itasimamishwa.

No comments:

Post a Comment