Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 19 December 2014

Matokeo ya uchaguzi TZ yaonesha kuimarika upinzani

Matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika juzi nchini Tanzania yanaonyesha kuimarika upinzani nchini humo baada ya kupata viti vingi vya uenyekiti wa mitaa na vijiji, pamoja na mamia ya wajumbe wa Serikali hizo.
Hayo yanaonyesha kuwa vyama hivyo vimeanza kuimarika katika ngazi za chini, tofauti na ilivyokuwa mwaka 2009, katika uchaguzi ambao CCM kilipata ushindi wa kishindo wa asilimia 91.72, huku wapinzani wakigawana asilimia 8.28 zilizobaki.
Licha ya uchaguzi huo wa juzi kugubikwa na kasoro nyingi, upinzani umeonekana kuchomoza huku katika baadhi ya mikoa ukipata ushindi maradufu hasa katika maeneo ambayo una nguvu kubwa wakati katika maeneo ambayo ulikuwa na viti vichache au kutokuwa navyo kabisa, umeibuka na kuipokonya CCM baadhi ya mitaa na vijiji.
Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) yaani Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi vimejizolea viti vingi tofauti na awali, huku chama kipya cha ACT kikichomoza na kupata ushindi katika maeneo kadhaa ya mikoa ya Kigoma na Katavi.
Mikoa ambayo upinzani umeonekana kuzoa viti vingi ni Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Kigoma, Mara, Kagera na Dar es Salaam, hali ambayo wachunguzi wa mambo wameielezea kuwa siyo dalili njema kwa CCM.

No comments:

Post a Comment