Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 12 December 2014

Sudan iko tayari kukabiliana na makundi ya waasi

Mkuu wa Kitengo cha Intelijinsia nchini Sudan amesisitiza kuwa vikosi vya usalama vya nchi hiyo vimewekwa tayari kwa lengo la kukabiliana na vita vya pande zote dhidi ya makundi ya waasi nchini humo. Muhammad Atta al Mauli amesema kuwa, ulinzi na usalama unapaswa kuimarishwa zaidi kwa lengo la kukabiliana na makundi ya waasi yanayoleta chokochoko katika majimbo mbalimbali ya nchi hiyo. Al Mauli ameongeza kuwa, vikosi vya usalama vimejizatiti katika maeneo ya majimbo ya Kordofan Kusini na Darfur kwa lengo la kukabiliana na mashambulizi hayo ya waasi. Amesema kuwa, baadhi ya makundi yanajaribu kuwavunja moyo wananchi kwa kusambaza fikra na propaganda potovu kwamba jeshi la Sudan halina uwezo wa kupambana na makundi ya waasi. Inafaa kuashiria hapa kuwa, majimbo ya Kordofan Kusini na Darfur yanakabiliwa na machafuko kwa karibu miaka mitatu sasa, tokea Sudan Kusini ilipojitenga na Sudan na kuwa taifa huru.

No comments:

Post a Comment