Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 12 December 2014

Dafina ya Kanali Gaddafi yafichuliwa Afrika Kusini

Duru za habari kutoka Afrika Kusini zimetangaza kufichuliwa utajiri mkubwa na dafina iliyofichwa wakati wa kipindi cha utawala wa dikteta Muammar Gaddafi wa Libya nchini humo. Gazeti la Independent Online la nchini Afrika Kusini limeandika kuwa, zaidi ya dola bilioni 200, mamia ya tani za dhahabu, vipande milioni sita vya almasi na vito vya thamani vilitoroshwa na utawala wa Gaddafi na kuhamishiwa nchini Afrika Kusini. Taarifa zinasema kuwa, mali zote zilizotoroshwa na utawala wa dikteta Gaddafi nchini Afrika Kusini zimehifadhiwa kwenye maghala saba, na zinafikia zaidi ya dola trilioni mbili. Gazeti hilo limeandika kuwa, Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini na serikali yake wanakabiliwa na mashinikizo makubwa ya jamii ya kimataifa kuhusiana na mali na utajiri huo mkubwa wa wananchi wa Libya uliofichwa nchini humo. Imeelezwa kuwa, hivi sasa dafina hiyo iliyoibiwa kutoka Libya na kufichwa katika eneo la siri lililoko katika maeneo ya kati ya Johannesburg na Pretoria ilisafirishwa kwa kutumia zaidi ya shehena 62 za ndege kutoka Libya na kupelekwa Afrika Kusini mwishoni mwa utawala wa dikteta Gaddafi

No comments:

Post a Comment