Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 19 December 2014

UN yatafuta milioni 810 kuwasaidia wakimbizi S/Kusini

Mashirika ya Kimataifa ya Kutoa Misaada ya Kibinadamu yanatafuta dola milioni 810 kwa ajili ya kuwasaidia wakimbizi wa Sudan Kusini ifikapo mwakani. Mkuu wa Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR ametahadharisha kwamba, iwapo mapigano hayatasimamishwa nchini Sudan Kusini na kufikiwa makubaliano ya amani, kuna uwezekano mkubwa wa kuongezeka idadi ya wakimbizi wa nchi hiyo kwenye kambi za wakimbizi zilizoko nchi jirani na kufikia idadi ya wakimbizi laki nane na elfu ishirini na moja. Mkuu wa Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR amezitaka nchi jirani na Sudan Kusini kushirikiana na shirika hilo la kimataifa kwa lengo la kuhifadhiwa usalama na maisha ya wakimbizi walioko kambini. Taarifa zinasema kuwa, wakimbizi wasiopungua elfu tisini na saba wanakabiliwa na hali mbaya kwenye kambi za Umoja wa Mataifa zilizoko nchini Sudan Kusini 'UNMISS'. Wakati huohuo, Amina Mohamed Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Biashara ya Kimataifa wa Kenya amewataka wafadhili wa kimataifa kutoa misaada yao ya kifedha kwa ajili ya kuzuia kujitokeza mgogoro wa kibinadamu nchini humo. Waziri Amina Mohamed amesisitizia udharura wa kukomeshwa mapigano na kurejeshwa amani na utulivu nchini Sudan Kusini.

No comments:

Post a Comment