Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 12 December 2014

Mauaji ya Waziri wa Palestina yachunguzwe haraka”

Mkuu mpya wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesisitiza juu ya udharura wa kufanyika uchunguzi wa haraka na huru kuhusiana na sababu ya kufa shahidi Ziad Abu Ein, Waziri Asiye na Wizara Maalumu wa Palestina. Federica Mogherini amebainisha kwamba, kuna haja ya kufanyika uchunguzi kuhusiana na sababu ya kifo cha waziri huyo. Aidha Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuna udharura kwa jamii ya kimataifa kuingilia kati kuhusiana na kile kinachojiri katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Wakati huo huo, Ban Ki-Moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa naye ameutaka utawala wa Kizayuni wa Israel ufanye uchunguzi kuhusiana na sababu ya kufa shahidi waziri huyo wa Palestina. Ikumbukwe kuwa, jana wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel walimuua shahidi Ziad Abu Ein, Waziri Asiye na Wizara Maalumu wa Palestina, kwenye vurugu zilizotokea kati ya askari wa Israel na wananchi wa Palestina katika kitongoji cha Turmus Ayya. Taarifa zinasema kuwa, wanajeshi wa Israel walianza kuwafyatulia gesi ya kutoa machozi Wapalestina waliokuwa wakipanda mizaituni kulalamikia ujenzi wa ukuta wa kidhalimu wa Israel katika eneo la Turmus Ayya lililoko kaskazini mwa Ramallah. Ziad Abu Ein ambaye alikuwemo kwenye maandamano ya Wapalestina ya kupinga ujenzi wa ukuta huo alipigwa na kitu kizito kichwani na kupoteza fahamu, na juhudi za kuokoa maisha yake zilishindikana kutokana na kuzidiwa na gesi.

No comments:

Post a Comment