Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 12 December 2014

Kenya yaimarisha usalama kukabiliana na al Shabab

Serikali ya Kenya imetangaza kuchukua hatua kali zaidi za kiusalama kwa lengo la kukabiliana na kundi la kigaidi la al Shabab la nchini Somalia. Taarifa kutoka Nairobi zinasema kuwa, hatua hiyo ya serikali ya Kenya imechukuliwa baada ya kushadidi mashambulio ya kundi la al Shabab nchini humo. Aidha serikali ya Kenya imeongeza muda wa kuwaweka rumande washukiwa wa ugaidi kutoka siku 90 hadi 360 pamoja na kusimamia kikamilifu idara ya mawasiliano nchini humo. Mpango huo pia umelenga kupunguza idadi ya wakimbizi wa kigeni walioko nchini humo na kufikia laki moja na nusu, ikilinganishwa na wakimbizi laki sita na elfu saba walioko hivi sasa kwenye kambi za wakimbizi nchini humo. Hali kadhalika, serikali ya Kenya imetangaza kuwa, waandishi wa habari ambao watapatwa na hatia ya kuzuia kufanyika uchunguzi na operesheni za kupambana na ugaidi watahukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela. Hali kadhalika, waandishi wa habari watakaotumia suhula za kijamii kwa lengo la kuwashawishi wananchi kutekeleza operesheni za kigaidi watahukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka ishirini jela. Inafaa kuashiria hapa kuwa, serikali ya Kenya inakabiliwa na mashinikizo makubwa yanayotokana na mashambulio ya kigaidi, tokea kiliposhambuliwa kituo cha kibiashara cha Westgate jijini Nairobi mwezi Septemba mwaka jana, na kupelekea watu wasiopungua 67 kuuawa. Mapema mwezi huu, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya aliwafuta kazi Waziri wa Mambo ya Ndani pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi baada ya kuongezeka mashambulio ya kundi la kigaidi la al Shabab katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo

No comments:

Post a Comment