Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Tuesday, 9 December 2014

Tunahitaji viongozi wazoefu au wabunifu?(2)


Kwa ufupi
Nane; Anayetambua na kuthamini jitihada za wengine. Kutambua jitihada za unaowaongoza na kuwapongeza ni jambo muhimu kwa kiongozi yeyote hasa wa jumuiya ya shule.
Uongozi ni mchakato wa ushawishi wa kijamii kwamba mtu mmoja anapopata madaraka huwasaidia wengine kukamilisha malengo ya pamoja.
Uongozi ni kuvuka mipaka ya mazoea na kuanzisha michakato ya mabadiliko ya kimapinduzi inayowaelekeza watu kufikia malengo kwa tija na ufanisi mkubwa.
Ni dhana na taaluma inayompa mhusika madaraka na uwezo wa kuwawezesha wale wanaongozwa kuunganisha nguvu, stadi na vipaji vyao na kuvitumia ili kufikia malengo yao.
Uongozi ni mchakato wa kuonyesha maana ya kile watu wanafanya kwa pamoja ili watu waelewe na kujituma zaidi kufikia malengo.
Wiki iliyopita tulichambua baadhi ya sifa sita za kiongozi bora. Leo tunaendelea.
Saba; Jasiri wa kufanya uamuzi sahihi, wenye tija na kusimamia utekelezaji. Awe na utayari wa kutekeleza wajibu wake pasipo kuyumbishwa wala kuogopa vitisho vya watu, hasa anapojua kwamba anachofanya kipo sahihi kisheria na kimebeba maslahi ya umma mpana.
Hii inahusisha kuwa tayari kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya watu wake. Viongozi kama hawa kwa sasa ni wachache. Mtu asiye na ujasiri wa kufanya amuzi sahihi huyu hafai kuwa kiongozi wa kisiasa au wa kitaaluma.
Nane; Anayetambua na kuthamini jitihada za wengine. Kutambua jitihada za unaowaongoza na kuwapongeza ni jambo muhimu kwa kiongozi yeyote hasa wa jumuiya ya shule.
Walimu wanaofanya kazi kwa jitihada kubwa na kujituma wanapaswa kutambuliwa, kuthaminiwa, kutiwa moyo na kupongezwa. Vivyo hivyo, wanafunzi wenye jitihada kubwa na wanaojituma kusoma kwa bidii wanapaswa kutambuliwa, kutiwa moyo na kupongezwa.
Kwa bahati mbaya shule zetu nyingi zinatambua jitihada za wanafunzi, lakini zimewasahau walimu wenye jitihada kubwa na wanaojituma kufikia malengo. Kiongozi makini anapaswa kufahamu hili na kulitekeleza kikamilifu.
Tisa; Mwenye maarifa na anayependa kujifunza zaidi. Kila siku maarifa mapya na teknolojia mpya inaibuka duniani. Kiongozi bora ni yule anayechangamkia fursa ya kujifunza.
Anachangamkia kupata maarifa zaidi kwenye kazi zake za uongozi, kwenye sera na mipango ya nchi, kwenye mikakati ya kitaifa na masuala nyeti ya kitaifa yanayomhusu. Kuwa na maarifa kuna faida kubwa katika jukumu la uongozi.

No comments:

Post a Comment