Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 12 December 2014

Ayatullah Khatami: Mateso ya CIA ni unyama mkubwa

Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa hapa mjini Tehran amesema leo kuwa, ripoti iliyotolewa wiki hii na Baraza la Seneti nchini Marekani ni ya kushtua. Ripoti hiyo imefichua jinsi Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) lilivyowatesa kinyama washukiwa wa ugaidi katika jela la Guantanamo miaka kadhaa iliyopita. Ayatullah Ahmad Khatami amesema mateso hayo ya CIA dhidi ya washukiwa wa ugaidi ni unyama na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu. Ayatullah Khatami amesema inasikitisha kuona Marekani ikijigamba kuwa inatetea haki za binadamu duniani ilihali nchi hiyo ndiyo mkiukaji nambari moja wa haki hizo. Khatibu wa Sala ya Ijumaa hapa Tehran pia amelaani mauaji ya Waziri wa Palestina, Ziad Abu Ein aliyeuawa shahidi siku ya Jumatano na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel. Ayatullah Ahmad Khatami amesema serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Palestina inapaswa kuchukua hatua kali dhidi ya Israel kufuatia jinai hiyo. Amesema kwa mara nyingine tena Wazayuni wameonyesha udhalimu na unyama wao hadharani na kusisitiza kuwa muqawama na mapambano ya Wapalestina ndiyo njia pekee ya kumshinda adui mzayuni.

No comments:

Post a Comment