Uchaguzi wa urais nchini Nigeria unatarajiwa kuwa na ushindani
mkubwa na wa aina yake baada ya vyama vikuu kuwachagua wagombea wao.
Chama tawala cha PDP kimemteua Rais Goodluck Jonathan kuwa mgombea wake
huku muungano mkuu wa upinzani wa APC ukimteua rais wa zamani, Jenerali
Mohammadu Buhari kupeperusha bendera yake kwenye uchaguzi unaotarajiwa
kufanyika Februari 15 mwakani. Buhari amemshinda mpinzani wake wa
karibu, Atiku Abubakar, ambaye ni makamu wa zamani wa rais wa nchi hiyo
kwenye uchaguzi wa ndani wa APC uliofanyika hapo jana.
Kampeni za uchaguzi zinatarajiwa kuwa ngumu hasa kwa upande wa chama tawala kutokana na serikali kuonekana kushindwa kudhibiti kundi la kigaidi la Boko Haram. Pia serikali ya Rais Jonathan itakuwa na kibarua kigumu kuwashawishi wapiga kura kwani inatuhumiwa kuhusika na ufisadi. Wajuzi wa mambo wanasema Jenerali Buhari ana sifa nzuri ya kupambana na ufisadi kwani alipoingia madarakani 1983 kupitia mapinduzi ya kijeshi alichukua hatua muhimu kukabiliana na uozo huo kabla ya kuondolewa madarakani 1985 kwenye mapinduzi mengine ya kijeshi yaliyoongozwa na Ibrahim Babangida
Kampeni za uchaguzi zinatarajiwa kuwa ngumu hasa kwa upande wa chama tawala kutokana na serikali kuonekana kushindwa kudhibiti kundi la kigaidi la Boko Haram. Pia serikali ya Rais Jonathan itakuwa na kibarua kigumu kuwashawishi wapiga kura kwani inatuhumiwa kuhusika na ufisadi. Wajuzi wa mambo wanasema Jenerali Buhari ana sifa nzuri ya kupambana na ufisadi kwani alipoingia madarakani 1983 kupitia mapinduzi ya kijeshi alichukua hatua muhimu kukabiliana na uozo huo kabla ya kuondolewa madarakani 1985 kwenye mapinduzi mengine ya kijeshi yaliyoongozwa na Ibrahim Babangida
No comments:
Post a Comment