Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Friday, 12 December 2014

Waziri wa Palestina aliyeuawa shahidi na Israel azikwa

Waziri wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Palestina aliyeuawa shahidi kwa kupigwa hapo jana na mwanajeshi wa utawala haramu wa Israel amezikwa leo. Maelfu ya Wapalestina wakiongozwa na Rais Mahmoud Abbas wamehudhuria maziko ya Ziad Abu Ein huku waombolezaji wakimtaka Abbas achukue hatua kali dhidi ya utawala ghasibu wa Israel. Hapo jana madaktari walioupasua mwili wa Abu Ein kwa ajili ya kuchunguza chanzo cha kifo chake walisema kiongozi huyo alipoteza maisha baada ya kupata majeraha shingoni pamoja na kuvuta gesi yenye sumu. Utawala wa Kizayuni wa Israel umekataa kutambua ripoti ya madaktari licha ya kuwepo mwakilishi wake kwenye shughuli za upasuaji wa mwili wa Waziri Ziad. Utawala huo bandia umetoa taarifa ya upotoshaji na kusema Ziad Abu Ein alifariki dunia kutokana na mshituko wa moyo. Picha za video zinazoonyesha jinsi mwanajeshi mzayuni alivyomkaba koo waziri huyo wa Palestina zimesambaa katika mitandao ya kijamii na hivyo kuamsha hasira za ulimwengu kuhusiana na jinai hiyo ya Israel. Umoja wa Ulaya, Umoja wa Mataifa pamoja na nchi mbalimbali za dunia zikiwemo Iran na Russia zimelaani mauaji ya Waziri huyo na kutaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wale waliohusika na unyama huo.

No comments:

Post a Comment