Zoezi la upigaji kura linaendelea nchini Burundi na tayari
kumeripotiwa kutokea mashambulizi katika vituo kadhaa vya kupigia kura.
Wapiga kura wanaripotiwa kuwa wachache katika uchaguzi huo wa bunge
na serikali za mitaa huku watu wengi wakionekana kuhofia kujitokeza
katika vituo vya kupigia kura. Uchaguzi huo unafanyika pamoja na kuwa
jamii ya kimataifa imeitaka serikali ya Burundi kuuahirisha na kupanga
wakati mwingine unaokubalika na pande zote husika na chaguzi nchini
humo.
Wapinzani Burundi wametangaza kususia uchaguzi kwa madai kuwa si huru
na wa haki. Burundi ilitumbukia katika mgogoro mkubwa wa kisiasa
kuanzia mwezi Aprili wakati Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza uamuzi
wake wa kugombea kiti cha urais kwa muhula wa tatu. Zaidi ya watu 70
wamepoteza maisha katika machafuko ya kabla ya uchaguzi Burundi huku
wengine zaidi ya laki moja wakikimbia nchi
No comments:
Post a Comment