Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 29 June 2015

Upigaji kura waanza nchini Burundi, ghasia zaripotiwa

Zoezi la upigaji kura linaendelea nchini Burundi na tayari kumeripotiwa kutokea mashambulizi katika vituo kadhaa vya kupigia kura.
Wapiga kura wanaripotiwa kuwa wachache katika uchaguzi huo wa bunge na serikali za mitaa huku watu wengi wakionekana kuhofia kujitokeza katika vituo vya kupigia kura. Uchaguzi huo unafanyika pamoja na kuwa jamii ya kimataifa imeitaka serikali ya Burundi kuuahirisha na kupanga wakati mwingine unaokubalika na pande zote husika na chaguzi nchini humo.
Wapinzani Burundi wametangaza kususia uchaguzi kwa madai kuwa si huru na wa haki. Burundi ilitumbukia katika mgogoro mkubwa wa kisiasa kuanzia mwezi Aprili wakati Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza uamuzi wake wa kugombea kiti cha urais kwa muhula wa tatu. Zaidi ya watu 70 wamepoteza maisha katika machafuko ya kabla ya uchaguzi Burundi huku wengine zaidi ya laki moja wakikimbia nchi

No comments:

Post a Comment